• HABARI MPYA

    Saturday, July 07, 2012

    MAMBO YAIVA KAGAME CUP 2012


    Mabingwa watetezi, Yanga SC

    Na Prince Akbar
    KLABU za AS Vita Club ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) na URA ya Uganda zinatarajia kuwasili nchini Julai 12 mwaka huu kushiriki michuano ya Klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame) itakayofanyika Dar es Salaam kuanzia Julai 14 mwaka huu.
    Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniphace Wambura Mgoyo ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba AS Vita Club ambayo iko kundi A pamoja na timu za Simba (Tanzania Bara), Ports (Djibouti) na URA itawasili saa 1.20 usiku kwa ndege ya Kenya Airways ikipitia Nairobi.
    Nayo URA itatua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jioni ya siku hiyo kwa ndege ya Air Uganda. AS Vita imepangiwa kufikia hoteli ya Rombo Green View wakati URA itakuwa hoteli ya Royal Valentino.
    Katika michuano hiyo, mabingwa watetezi Yanga watafungua dimba na Atletico ya Burundi katika mchezo wa Kundi C Julai 14, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, wakati wapinzani wao wa jadi, Simba SC waliowekwa Kundi A, wataanza na URA ya Uganda Julai 16, kwenye Uwanja huo huo.
    Wawakilishi wengine wa Tanzania katika michuano hiyo, Azam FC wao wataanza na Mafunzo ya Zanzibar katika mchezo wa Kundi B, Uwanja wa Chamazi, Julai 15.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAMBO YAIVA KAGAME CUP 2012 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top