| Kocha mpya wa timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, Mholanzi Mart Nooij akiiongoza timu hiyo jana katika mchezo wa kwanza wa mchujo kuwania kupangwa kwenye makundi ya kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika mwaka 2015 nchini Morocco. Nooij, ambaye anafanana na mcheza mieleka maarufu wa zamani, Terry Gene Bolllea maarufu kama Hulk Hogan wa Marekani alianza vizuri jana mchezo wa kwanza wa mashindano kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya Zimbabwe Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Picha ya ni Hulk Hogan. |
0 comments:
Post a Comment