Na Mahmoud Zubeiry, Dar es Salaam
WINGA aliyekuwa akimsumbua Shomary Kapombe upande wa kushoto wa Uwanja jana, Kudakwashe Mahachi ameomba mshahara wa dola za Kimareakni 1,000 kwa klabu yoyote ya Tanzania itakayotaka kumsajili pamoja na ada ya kusaini.
Winga huyo wa chipukizi wa Zimbabwe amesema kwa kuwa yeye bado kijana mdogo hataki mshahara mkubwa kucheza Tanzania, bali dola 1,000 kwa mwezi itamtosha.
“Niko tayari kujiunga na klabu yoyote ya Tanzania kwa mshahara wa doa 1,000 tu, naondoka kurudi Zimbabwe ila timu ambayo imevutiwa na mimi inaweza kunifuata tumalizane,”alisema mchezaji huyo wa Chicken Inn F.C.
Bao pekee la mshambuliaji wa Azam FC, John Bocco ‘Adebayor’ jana dakika ya 13 akimalizia krosi ya Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe ya DRC liliipa Taifa Stars ushindi wa 1-0 dhidi ya Zimbabwe katika mchezo huo.
Ushindi huo mwembamba unaipa Taifa Stars mzigo wa kwenda kucheza kwa nidhamu ya hali ya juu kwenye mchezo wa marudiano Juni 1, ili kuingia hatua ya mwisho ya mchujo kuwania nafasi ya kuingia kwenye makundi ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika mwaka 2015 nchini Morocco.
WINGA aliyekuwa akimsumbua Shomary Kapombe upande wa kushoto wa Uwanja jana, Kudakwashe Mahachi ameomba mshahara wa dola za Kimareakni 1,000 kwa klabu yoyote ya Tanzania itakayotaka kumsajili pamoja na ada ya kusaini.
Winga huyo wa chipukizi wa Zimbabwe amesema kwa kuwa yeye bado kijana mdogo hataki mshahara mkubwa kucheza Tanzania, bali dola 1,000 kwa mwezi itamtosha.
![]() |
Dola 1,000 unabeba kifaa; Winga wa Zimbabwe, Kudakwashe Mahachi ameomba mshahara wa dola 1,000 tu acheze Tanzania |
![]() |
Mahachi akishangilia moja ya mabao aliyowahi kuifungia Zimbabwe |
“Niko tayari kujiunga na klabu yoyote ya Tanzania kwa mshahara wa doa 1,000 tu, naondoka kurudi Zimbabwe ila timu ambayo imevutiwa na mimi inaweza kunifuata tumalizane,”alisema mchezaji huyo wa Chicken Inn F.C.
Bao pekee la mshambuliaji wa Azam FC, John Bocco ‘Adebayor’ jana dakika ya 13 akimalizia krosi ya Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe ya DRC liliipa Taifa Stars ushindi wa 1-0 dhidi ya Zimbabwe katika mchezo huo.
Ushindi huo mwembamba unaipa Taifa Stars mzigo wa kwenda kucheza kwa nidhamu ya hali ya juu kwenye mchezo wa marudiano Juni 1, ili kuingia hatua ya mwisho ya mchujo kuwania nafasi ya kuingia kwenye makundi ya kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Mataifa ya Afrika mwaka 2015 nchini Morocco.
0 comments:
Post a Comment