Nassor Masoud 'Chollo' wa Simba akitia krosi katika mechi ya jana |
Na Prince Akbar
MECHI ya Ligi Kuu ya Vodacom kuwania ubingwa wa Tanzania Bara
kati ya Simba na African Lyon iliyochezwa jana (Septemba 15 mwaka huu) Uwanja
wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 67,793,000.
Washabiki 11,505 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo ambapo
viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000. Kila timu
ilipata sh. 14,603,263.47 wakati asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani
(VAT) iliyokatwa ni sh. 10,341,305.08.
Mgawo mwingine umekwenda kwa msimamizi wa kituo sh. 20,000,
posho ya kamishna wa mechi sh. 114,000, mwamuzi wa akiba sh. 70,000, et iti.sh.
3,175,000, vishina kwenye tiketi (attachments) sh. 345,150, maandalizi ya
uwanja (pitch preparation) sh. 400,000 na Wachina (stadium technical support)
sh. 2,000,000.
Umeme sh. 300,000, ulinzi na usafi uwanjani sh. 2,350,000,
Kamati ya Ligi sh. 4,867,754.49, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh.
2,920,652.69, uwanja sh. 4,867,754.49, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es
Salaam (DRFA) sh. 1,947,101.86, gharama za mchezo sh. 4,867,754.49.
Nayo mechi ya ligi hiyo kati ya Tanzania Prisons na Yanga
iliyochezwa jana (Septemba 15 mwaka huu) Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini
Mbeya imeingiza sh. 50,435,000.
Aidha, watazamaji 112 ndiyo waliokata tiketi kushuhudia mechi
ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya JKT Ruvu na Ruvu Shooting iliyofanyika jana
(Septemba 15 mwaka huu) Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.
Mapato yaliyopatikana katika mechi hiyo ambapo viingilio
vilikuwa sh. 3,000 na sh. 10,000 ni 340,000. Mgawo ulikuwa kama ifuatavyo; kila
timu sh. 29,465.87, asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh.
51,864.40, maandalizi ya uwanja sh. 100,000 na tiketi sh. 89,916.
Kamati ya Ligi sh. 9,821.95, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa
Miguu (FDF) sh. 5,893.17, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA)
sh. 3,928.78, gharama za mchezo sh. 9,821.95 na uwanja sh. 9,821.95.
0 comments:
Post a Comment