• HABARI MPYA

    Friday, September 28, 2012

    BOBAN BADO HASOMEKI ZANZIBAR

    Mtaalamu Boban

    Na Mahmoud Zubeiry
    LABDA leo, lakini jana wamemsubiri hadi boti ya mwisho hakushuka. Haruna Moshi Shaaban, mchezaji pekee ambaye hayupo kambini Simba SC, alitarajiwa kuungana na wenzake jana, visiwani Zanzibar kwa maandalizi ya mchezo dhidi ya wapinzani wao wa jadi, Yangas SC, lakini wapi.
    Sasa uongozi wa Simba utamsikilizia mchezaji huyo leo kama atatimiza wajibu wake na tofauti na hapo, watachukua.  
    Boban hakucheza mechi iliyopita ya Ligi Kuu kati ya Simba na Ruvu Shooting, kwa sababu alikuwa anaumwa na hakwenda kambini wenzake, kwa kuwa alikuwa anajisikilizia afya yake, ila kuanzia jana alitarajiwa kuungana na wenzake kambini.
    Kuna uwezekano mkubwa Boban akapanda boti na wenzake na baada ya mechi ya kesho, dhidi ya Prisons.
    Japo Boban hayupo kambini Zanzibar, lakini Simba SC inaendelea vizuri na maandalizi yake ya pambano dhidi ya watani wao wa jadi, Yanga SC, Oktoba 3, mwaka huu, ikifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Chuo cha Kiislam, Kwerekwe, visiwani Zanzibar na kambi yao ipo Chukwani.
    Morali ya kambi ipo juu na wachezaji wote wako fiti, wakijifua kwa shauku kubwa ili kumvutia kocha Mserbia, Milovan Cirkovick awape nafasi ya kucheza Oktoba 3, kuanzia sa 1:00 usiku.
    Simba itarejea Dar es Salaam kesho kucheza mechi na Prisons ya Mbeya Uwanja wa Taifa, kisha kurejea tena visiwani humo kuendelea na maandalizi ya mchezo wa Jumamosi ijayo.
    Hata hivyo, katika michezo miwili ijayo, Simba itamkosa mshambuliaji wake Mganda, Emmanuel Okwi ambaye amefungiwa na Kamati ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, chini ya Mwenyekiti wake, Wallace Karia, sambamba na kumtoza faini ya Sh. 500,000 kwa kosa la kumpiga kiwiko mchezaji wa JKT Ruvu, Kessy Mapande.
    Okwi alifanya hivyo akilipa kisasi cha kuchezewa rafu Jumatano iliyopita, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
    Tayari Okwi amekosa mechi moja dhidi ya Ruvu Shooting na wakati, na sasa atakosa mechi mbili zaidi, dhidi ya Prisons na dhidi ya Yanga na baada ya hapo atakuwa huru kuendelea kumtumikia mwajiri wake.
    Siyo siri, kuelekea pambano la watani wa jadi, Okwi alikuwa ni homa kwa Yanga, hasa wakikumbuka namna alivyowanyanyasa katika mechi iliyopita, akifunga mabao mawili kwenye ushindi wa 5-0 na kusababisha mawili.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BOBAN BADO HASOMEKI ZANZIBAR Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top