• HABARI MPYA

    Sunday, September 30, 2012

    KUELEKEA PAMBANO LA WATANI; MARA NYINGI YANGA HUFUNGWA USIKU

    Kutoka kulia; Emmanuel Okwi, Patrick Mafisango (marehemu) na Felix Sunzu wakishangilia bao la penalti alilofunga Sunzu katika mechi ya mwisho ya usiku kukutanisha miamba hiyo. Simba ilishinda 2-0 Agosti 17, mwaka jana Uwanja wa Taifa, je, Jumatano itakuwaje?

    Na Mahmoud Zubeiry
    MECHI ya Jumatano ya watani wa jadi, Simba na Yanga itaanza saa 11:00 jioni na itamalizika kuanzia saa 1:00, wakati giza limekwishaingia uwanjani. Je, unajua matokeo ya mechi zilizopita za watani zilizoishia gizani? BIN ZUBEIRY yupo kwa ajili yako, pata vituz.

    MATOKEO YA MECHI ZA WATANI USIKU:
    JANUARI 1975
    Yanga Vs Simba; Fainali, 2-0
    WAFUNGAJI: Gibson Sembuli na Sunday Manara
    Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati

    JANUARI 1992
    Simba Vs Yanga; Fainali
    1-1, Simba ilishinda kwa penalti 5-4
    Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati

    JANUARI 12, 2011
    Simba Vs Yanga; Fainali 2-0
    WAFUNGAJI: Mussa Mgosi dk 33, Shijja Mkinna dk 71
    (Uwanja wa Amaan, Zanzibar)
    Kombe la Mapinduzi

    OKTOBA 27, 1992
    Simba v Yanga
    1-0
    MFUNGAJI: Damian Morisho Kimti.
    Ligi ya Muungano

    AGOSTI 17, 2011
    Simba vs Yanga 2-0, Dar
    WAFUNGAJI:
    Haruna Moshi ‘Boban’ dk 15 na Felix Sunzu dk 38.
    Ngao ya Jamii
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KUELEKEA PAMBANO LA WATANI; MARA NYINGI YANGA HUFUNGWA USIKU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top