• HABARI MPYA

    Friday, September 21, 2012

    MTAKATIFU TOM AMTEMA BAHANUZI, AMCHUKUA TEGETE MECHI YA KESHO NA JKT

    Saintfiet akipanda basi jipya la Yanga baada ya kumaliza kuzungumza na Waandishi wa Habari mchana wa leo makao makuu ya klabu, Jangwani.

    Na Mahmoud Zubeiry
    KOCHA Mkuu wa Yanga SC, Mbelgiji Tom Saintefiet ameteua wachezaji 18 kwa ajili ya mchezo wa kesho wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, dhidi ya JKT Ruvu, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, safari hii akimchukua mshambuliaji Jerry Tegete na kumtema Said Bahanuzi.
    Akizungumza na Waandishi wa Habari mchana wa leo makao makuu ya klabu, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Dar es Salaam, Mbelgiji huyo alisema anaelekea kukatishwa tamaa na wachezaji wake hivi sasa juu ya viwango vyao.
    Alisema hata kufunga penalti, hivi sasa imekuwa ni tatizo na mazoezini jana akiwajaribu kwa penalti wachezaji wake, kati ya mastaa wake sita, waliofunga ni wawili tu. “Yaani hata kesho siombei nipate penalti, maana sijui kama tutaweza kuitumia vizuri,”alisema Mtakatifu Tom.
    Aliwataja wachezaji aliowateua kwa ajili ya mechi ya kesho, ambayo itakuwa ya tatu tangu kuanza kwa Ligi Kuu ni makipa; Yaw Berko, Ally Mustafa ‘Barthez’, mabeki Juma Abdul, Godfrey Taita, Mbuyu Twite, Kevin Yondan,  Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Ladislaus Mbogo, Oscar Joshua na Stefano Mwasyika.
    Aliwataja viungo ni Athumani Iddi ‘Chuji’, Haruna Niyonzima, Nizar Khalfan, Rashid Gumbo, Shamte Ally na Simon Msuva, wakati washambuliaji ni Jerry Tegete, Didier Kavumbangu na Hamisi Kiiza na ambao hawamo kwenye programu ya kesho ni kipa Said Mohamed, mabeki Nsajigwa Shadrack, Job Ibrahim, viungo Frank Domayo, Juma Seif ‘Kijiko’, Salum Telela, Omega Seme, Nurdin Bakari, Idrisa Assega, na Issa Ngao wa Yanga B anayekomazwa kikosi cha kwanza na mshambuliaji Said Bahanuzi.
    Yanga imeambulia pointi moja tu katika mechi zake mbili za Ligi Kuu, awali ikilazimishwa sare ya bila kufungana na Prisons kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya Jumamosi na Jumatano ikachapwa mabao 3-0 Morogoro Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.
    Huo ulikuwa mchezo wa pili Saintfiet anafungwa Yanga katika mechi 14 alizoiongoza timu hiyo tangu ajiunge nayo, Julai mwaka huu, akirithi mikoba ya Mserbia, Kostadin Bozidar Papic.
    Katika mechi hizo, zimo sita za Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, ambazo aliiwezesha Yanga kutwaa taji, ikipoteza mechi moja tu dhidi ya Atletico ya Burundi.  

    REKODI YA SAINTFIET YANGA
    1.     Yanga Vs JKT Ruvu             (Kirafiki)                    2-0
    2.     Yanga Vs Atletico (Burundi, Kagame)               0-2
    3.     Yanga Vs Waw Salam (Sudan, Kagame)          7-1
    4.     Yanga Vs APR (Rwanda, Kagame)                     2-0
    5.     Yanga Vs Mafunzo (Z’bar, Kagame)                 1-1 (5-3penalti)
    6.     Yanga Vs APR (Rwanda, Kagame)                     1-0
    7.     Yanga Vs Azam (Kagame)                                    2-0
    8.     Yanga Vs African Lyon (Kirafiki)                         4-0
    9.     Yanga Vs Rayon (Kirafiki, Rwanda)                   2-0
    10.                        Yanga Vs Polisi (Kirafiiki, Rwanda)        2-1
    11.                        Yanga Vs Coastal Union    (Kirafiki)        2-1
    12.                        Yanga Vs Moro United      (Kirafiki)        4-0
    13.                        Yanga Vs Prisons    (Ligi Kuu)                  0-0
    14.                        Yanga Vs Mtibwa (Ligi Kuu)                     0-3
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MTAKATIFU TOM AMTEMA BAHANUZI, AMCHUKUA TEGETE MECHI YA KESHO NA JKT Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top