• HABARI MPYA

    Wednesday, September 12, 2012

    MUNDU YAFUNDISHWA SOKA CHUONI, YACHAPWA VIWILI LIGI KUU ZANZIBAR


    Na Ally Mohamed, Zanzibar
    LIGI Kuu ya Zanzibar, maarufu Zanzibar Grand Malt Premier League, imemaliza mzunguko wake wa kwanza jana kwa kushuhudia mechi moja iliyochezwa Uwanja wa Amaan, ikiwakutanisha Chuoni na Mundu kutoka Kaskazini mwa kisiwa cha Unguja.
    Mechi hiyo imemalizika kwa timu ya Chuoni kuibuka na ushindi wa mabao 2-1, mabao ya Chuoni yote mawili yakifungwa kipindi cha kwanza kupitia kwa Shaffii Hassan katika dakika ya 44, bao la pili likifungwa na Ahmed Malik katika dakika ya 44.
    Mundu, ambayo iliteremka daraja, lakini wakainunua Miembeni United iliyobaki Ligi Kuu, ilipata bao lake pekee kupitia kwa Mfanyeje Mussa, dakika ya 56.
    Ligi hiyo inatarajia kuendelea tena Jumamosi wiki hii kwa michezo miwili, kisiwani Pemba katika Uwanja wa Gombani, mabingwa watetezi wa ligi hiyo na wawakilishi wa Zanzibar katika Ligi ya Mabingwa Afrika, Super Falcon wakikipiga na Duma timu inayomilikiwa na Jeshi la Kujenga Uchumi la Zanzibar (JKU).
    Itakumbukwa kuwa mechi iliyopita Super Falcon walipoteza baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Chipukizi, huku Duma wakikubali kipigo kama hicho kutoka kwa wawakilishi wa Zanzibar katika kpmbe la Shirikisho, Jamhuri.
    Kisiwani Unguja katika Uwanja wa Amaan, mabaharia wa KMKM ambao walipoteza mchezo wao uliopita baada ya kukubali kipigo chembamba cha bao 1-0 kutoka kwa Mafunzo, watateremka uwanjani hapo kukabiliana na Malindi ambao nao katika mechi yao ya kwanza walipoteza dhidi ya Bandari baada ya kukubali kipigo cha mabao 3-2.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MUNDU YAFUNDISHWA SOKA CHUONI, YACHAPWA VIWILI LIGI KUU ZANZIBAR Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top