• HABARI MPYA

    Thursday, May 01, 2014

    TFF YATEUA WAKILI KUCHUNGUZA USAJILI WA DOMAYO AZAM FC

    Na Waandishi Wetu, Dar es Salaam
    KUTOKANA na tukio lililotokea jana (Aprili 30 mwaka huu) kwenye kambi ya timu ya Taifa (Taifa Stars) iliyopo Tukuyu mkoani Mbeya likihusisha usajili wa baadhi ya timu, Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amemteua Wakili Wilson Ogunde kuchunguza mlolongo mzima wa tukio hilo.
    Taarifa ya TFF kwa BIN ZUBEIRY leo asubuhi imesema kwamba, baada ya kukamilisha uchunguzi wake, Wakili Ogunde ataishauri TFF kuhusu hatua za kisheria na kikanuni za kuchukua.
    Frank Domayo akisaini Azam FC jana
    TFF imesema katika taarifa yake inatoa wito kwa wachezaji, klabu na wadau wa mpira wa miguu kufuata kanuni na taratibu katika utendaji wao.
    Viongozi wa Azam FC jana walikwenda kwenye kambi ya Taifa Stars kukamilisha taratibu za usajili na kiungo Frank Domayo, aliyemaliza Mkataba wake Yanga SC.
    Baada ya kufanikiwa kumsainisha Mkataba wa miaka miwili, wasimamizi wa kambi waliwaitia Polisi viongozi wa Azam FC ambao hata hivyo baadaye waliachiwa. Lakini inadaiwa fomu za usajili zilichanwa.
    Azam si klabu ya kwanza kusajili mchezaji katika kambi ya timu ya taifa, kwani vigogo wa soka nchini, Simba na Yanga ndiyo waasisi wa mchezo huo.
    Mwaka jana Simba SC walisaini Mkataba mpya na kiungo wao, Amri Kiemba akiwa katika kambi ya Taifa Stars, hoteli ya Tansoma mjini Dar es Salaam.
    Inaruhusiwa kwa wakubwa tu; Kiongozi wa Yanga SC, Seif Ahmed 'Magari' alimtoa kambi ya Taifa Stars, beki Kevin Yondan akiwa Simba SC na kumsainisha mwaka 2012.  

    Yanga SC iliwasajili Domayo kutoka JKT Ruvu, Kevin Yondan kutoka Simba SC wote wakiwa katika kambi ya Taifa Stars Dar es Salaam miaka miwili iliyopita. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TFF YATEUA WAKILI KUCHUNGUZA USAJILI WA DOMAYO AZAM FC Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top