![]() |
| Mtakatifu Tom kushoto akizungumza na Waandishi wa Habari mchana wa leo Jangwani. Kulia ni Katibu wa klabu, Celestine Mwesigwa |
Na Mahmoud Zubeiry
KOCHA Mkuu wa
Yanga, Mbelgiji Tom Saintfiet ameteua wachezaji 22 kwa ajili ya mechi ya
ufunguzi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, dhidi ya Prisons Jumamosi kwenye
Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.
Akizungumza na
Waandishi wa Habari mchana wa leo makao makuu ya klabu, Saintfiet alisema ameteua
wachezaji hao kulingana na mazingira ya mechi yenyewe na kwamba wachezaji
wengine wote waliobaki ni wazuri pia.
Aliwataja wachezaji
aliowateua ambao wanaondoka kesho asubuhi kuwa ni makipa; Yaw Berko, Ally Mustafa ‘Barthez’, mabeki Shadrack Nsajigwa,
Juma abdul, Godfrey Taita, Mbuyu Twite, Kevin Yondan, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, David Luhende, Oscar
Joshua na Stefano Mwasyika.
Aliwataja
viungo ni Athumani Iddi ‘Chuji’, Haruna Niyonzima, Frank Domayo, Rashid Gumbo, Nizar
khalfan, Shamte Ally na Simon Msuva, wakati washambuliaji ni Jerry Tegete,
Didier Kavumbangu, Said Bahanuzi na Hamisi Kiiza.
Aliwataja wachezaji
wa kikosi cha kwanza ambao hawatasafiri kwa ajili ya mechi hiyo kuwa ni kipa
Said Mohamed, Ladislaus Mbogo, Job Ibrahim, Juma Seif ‘Kijiko’, Salum Telela, Omega
Seme, Nurdin Bakari, Idrisa Assega na Issa Ngao wa Yanga B, ambaye anakomazwa
kikosi cha kwanza.
Jumamosi
Yanga ilicheza mechi ya mwisho ya kujipima nguvu kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu
na kushinda mabao 4-0 dhidi ya Moro united, Mrundi Didier Kavumbangu akifunga
mawili, mengine beki Juma Abdul na kiungo Shamte Ally.
“Kavumbangu
aliwahi kufunga pia tulipocheza na Sinza Stars, ninafurahia hilo, ni muhimu kwa
klabu kubwa, lakini pia wachezaji wengine wanaweza kufunga, Stefano Mwasyika,
Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Juma Abdul…tumecheza mechi 14 kabla ya ligi, zikiwemo
dhidi ya Sinza Stars na Kijitonyama Stars, tumefunga mabao 42 na tumefungwa
sita tu,”alisema Mtakatifu Tom.
Saintfiet alitaka
mechi moja dhidi ya timu inayocheza kama wapinzani wao wa kwanza katika Ligi
Kuu, Prisons na pia katika Uwanja mbaya kama ambao atachezea mechi ya kwanza ya
ligi hiyo, Sokoine mjini Mbeya na ndiyo maana timu hiyo ikacheza na Moro United
juzi kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Kijitonyama.
Saintfiet
ameridhika na kiwango cha timu na sasa anasema timu iko tayari kwa Ligi Kuu,
akianza na Prisons iliyorejea Ligi Kuu msimu huu kwenye Uwanja wa Sokoine, Septemba
15.
Hiyo ilikuwa mechi ya 11, Saintfiet anashinda
Yanga katika mechi 12 tangu ajiunge nayo miezi miwili iliyopita, mbali ya ziwe
za mazoezini dhidi ya Sinza Stars na Kijitonyama Stars.
Ndani ya mechi hizo kuna mechi sita za
Klabu Bingwa ya soka Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame, ambalo
aliiwezesha Yanga kutwaa ubingwa wa tano wa michuano hiyo, ikipoteza mechi moja
tu ya kwanza dhidi ya Atletico ya Burundi, kwa kufungwa 2-0, mabao yote ya Kavumbangu,
ambaye baadaye ikamsajili.
REKODI YA SAINTFIET YANGA
1.
Yanga
Vs JKT Ruvu 2-0
2.
Yanga
Vs Atletico (Burundi) 0-2
3.
Yanga
Vs Waw Salam (Sudan Kusini) 7-1
4.
Yanga
Vs APR (Rwanda) 2-0
5.
Yanga
Vs Mafunzo (Z’bar) 1-1 (5-3penalti)
6.
Yanga
Vs APR (Rwanda) 1-0
7.
Yanga
Vs Azam 2-0
8.
Yanga
Vs African Lyon 4-0
9.
Yanga
Vs Rayon (Rwanda) 2-0
10. Yanga
Vs Polisi (Rwanda) 2-1
11. Yanga
Vs Coastal Union 2-1
12. Yanga
Vs Moro United 4-0



.png)
0 comments:
Post a Comment