• HABARI MPYA

    Wednesday, July 13, 2016

    JERRY MURO ALIVYOMPLEKEA HAJJI MANARA 'MILIONI NA UPUUZI' ZA MATIBABU

    Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Yanga, Jerry Muro (wa tatu kushoto) akimkabidhi mchango wa fedha Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Simba, Hajji Manara (anayemfuatia kulia) kwa ajili ya matibabu ya macho leo nyumbani kwake, Magomeni, Dar es Salaam. Manara anatakiwa kwenda kufanyiwa matibabu ya macho India baada ya jicho lake moja kupoteza uwezo wa kuona. 
    Kulia ni Daktari wa michezo, Nassor Matuzya aliyeshika fedha wakati wa kumkabidhi Hajji
    Dk Matuzya akizungumza na Hajji kabla ya kumkabidhi fedha hizo Sh, 1,055,000 ambazo ni michango ya wana Yanga mbalimbali
    Hajji (kulia) ambaye anahitaji kiasi cha dola za Kimarekani 10,000 (zaidi ya Sh. Milioni 20) akizungumza na Muro (katikati) na mwingine ni mwanachama wa Yanga, maarufu kama Chicharito
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: JERRY MURO ALIVYOMPLEKEA HAJJI MANARA 'MILIONI NA UPUUZI' ZA MATIBABU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top