• HABARI MPYA

    Friday, September 07, 2012

    SIMBA NA AZAM KUCHANGIA TEMEKE HOSPITALI


    Na Mahmoud Zubeiry
    ASILIMIA tano ya mapato yatakayopatikana kwenye mechi ya Ngao ya Jamii (Community Shield) kati ya Simba na Azam Jumanne ijayo, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, yatakwenda kwenye Hospitali ya Temeke mkoani Dar es Salaam.
    Ofisa wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniphace wambura Mgoyo ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba, kabla ya kukabidhi fedha hizo, na shirikisho hilo litakutana na uongozi wa Hospitali ya Temeke kupanga maeneo ambayo fedha hizo zitatumika kwenye hospitali hiyo.
    Mechi hiyo ya uzinduzi rasmi wa msimu wa 2012/2013 itakayoanza saa 10:00 jioni, viingilio vitakuwa sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya bluu na kijani, sh. 10,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 15,000 kwa viti vya VIP C na B wakati VIP A itakuwa sh. 20,000.
    Kihistoria hiyo itakuwa mechi ya tano ya Ngao ya Jamii kuchezwa nchini na ya pili kukutanisha timu nje ya wapinzani wa jadi wa soka ya Tanzania, Simba na Yanga.
    Mtibwa ilicheza na Yanga mwaka 2009, baada ya Simba kugoma na ikashinda mabao 2-1 na kutwaa Ngao, wakati kabla ya hapo, mwaka 2001, Ligi Kuu ya Tanzania ikiwa bado inadhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia bia ya Safari Lager, ilichezwa mechi ya kwanza ya Ngao kihistoria.
    Katika mechi hiyo, Yanga ilishinda mabao 2-1 dhidi ya Simba na mwaka juzi Yanga iliifunga tena Simba kwa penali 3-1 kufuatia sare ya 0-0 na mwaka jana, Simba ilitwaa Ngao ya kwanza katika historia yake, kwa kuifunga Yanga mabao 2-0. 

    MABINGWA WA MECHI ZA NGAO YA JAMII:
    Mwaka          Mshindi   Matokeo
    2001               Yanga       2-1 Simba
    2010               Yanga       0-0 Simba (3-1penalti)
    2011               Simba       2-0 Yanga
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA NA AZAM KUCHANGIA TEMEKE HOSPITALI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top