Na Mwandishi Wetu, MBEYA
BEKI wa kati Rajab Zahir aliyekuwa akicheza kwa mkopo Stand United kutoka Yanga SC ya Dar es Salaam amejiunga na Mbeya City FC leo.
Kwenye ofisi za City zilizopo Mkapa Hall, eneo la Soko Matola mjini hapa, Zahir amesaini Mkataba wa mwaka mmoja kujunga na kikosi cha kocha Mmalawi Kinnah Phiri na kusema kwamba ana imani kubwa ya kupata mafanikio yake kisoka akiwa na chini ya kocha huyo bora barani.
“Ninamshukuru Mungu kwa kuniwezesha kujiunga na City, hii ni moja kati ya timu kubwa nchini kwa sababu ina ushawishi wa kutosha kwenye soka la nchini yetu, kitu muhimu ni kuomba ushirikiano kutoka kwa pande zote kwa maana ya uongozi wachezaji wenzangu na mashabiki, hayo yote yatatufanya kutimiza malengo kwa sababu kila mmoja anahitaji mafanikio katika kazi kwangu mimi hapa ndiyo sehemu ambayo nitayapata” alisema.
Zahir amejiunga na City baada ya msimu mmoja wa mkopo kwa Stand United ya Shinyanga uliohitimisha kandarasi yake ya miaka mitatu na kikosi cha Yanga ya Dar es Salaam.
Akiwa Stand United, Zahir alifanikiwa kucheza michezo 23 katika mechi zote 30 zilizochezwa na timu hiyo ya Shinyanga na kufanikiwa kushika nafasi ya 7 ikikusanya jumla ya pointi 40 mwisho wa msimu uliopita.
Wakati huo huo: Mbeya City FC imekwenda kuweka kambi Kyela kwa siku 10 kabla ya kuhamia Malawi kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
BEKI wa kati Rajab Zahir aliyekuwa akicheza kwa mkopo Stand United kutoka Yanga SC ya Dar es Salaam amejiunga na Mbeya City FC leo.
Kwenye ofisi za City zilizopo Mkapa Hall, eneo la Soko Matola mjini hapa, Zahir amesaini Mkataba wa mwaka mmoja kujunga na kikosi cha kocha Mmalawi Kinnah Phiri na kusema kwamba ana imani kubwa ya kupata mafanikio yake kisoka akiwa na chini ya kocha huyo bora barani.
“Ninamshukuru Mungu kwa kuniwezesha kujiunga na City, hii ni moja kati ya timu kubwa nchini kwa sababu ina ushawishi wa kutosha kwenye soka la nchini yetu, kitu muhimu ni kuomba ushirikiano kutoka kwa pande zote kwa maana ya uongozi wachezaji wenzangu na mashabiki, hayo yote yatatufanya kutimiza malengo kwa sababu kila mmoja anahitaji mafanikio katika kazi kwangu mimi hapa ndiyo sehemu ambayo nitayapata” alisema.
Rajab Zahir akiwa na jezi ya Mbeya City baada ya kusaini leo |
Akiwa Stand United, Zahir alifanikiwa kucheza michezo 23 katika mechi zote 30 zilizochezwa na timu hiyo ya Shinyanga na kufanikiwa kushika nafasi ya 7 ikikusanya jumla ya pointi 40 mwisho wa msimu uliopita.
Wakati huo huo: Mbeya City FC imekwenda kuweka kambi Kyela kwa siku 10 kabla ya kuhamia Malawi kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
0 comments:
Post a Comment