TIMU ya Marekani imekamilisha idadi ya timu zote wenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia kutolewa baada ya jana kufungwa mabao 4-1 na Ubelgiji katika mchezo wa Hatua ya 16 Boora Uwanja wa Lumen Field Jijini Seattle, Washington nchini Marekani.
Mshambuliaji wa Atalanta ya Italia, Charles Marc S. De Ketelaere aliifungia mabao mawili Ubelgiji dakika ya tisa na 33, huku mabao mengine yakifungwa na kiungo mshambuliaji wa Club Brugge ya kwao, Hans Vanaken dakika ya 57 na mshambuliaji Romelu Lukaku Bolingoli mwenye asili ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) dakika ya 90’+3.
Bao pekee la na kufutia machozi la Marekani ambayo inaungama na wenyeji wenza wake Canada na Mexico kuaga michuano hiyo limefungwa na kiungo wa Bayer Leverkusen ya Ujerumani, Malik Leon Tillman dakika ya 31 na sasa Ubelgiji itakutana na Hispania katika Nusu Fainali ‘Tamu Kabisa’ Julai 10 Uwanja wa Hard Rock, Miami Gardens, Florida, Marekani.
Bao pekee la na kufutia machozi la Marekani ambayo inaungama na wenyeji wenza wake Canada na Mexico kuaga michuano hiyo limefungwa na kiungo wa Bayer Leverkusen ya Ujerumani, Malik Leon Tillman dakika ya 31 na sasa Ubelgiji itakutana na Hispania katika Nusu Fainali ‘Tamu Kabisa’ Julai 10 Uwanja wa Hard Rock, Miami Gardens, Florida, Marekani.



.png)
0 comments:
Post a Comment