// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); SIMBA SC UCHAGUZI JUNI 29 - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE SIMBA SC UCHAGUZI JUNI 29 - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Wednesday, May 07, 2014

    SIMBA SC UCHAGUZI JUNI 29

    Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
    UCHAGUZI mkuu wa Simba SC sasa umepangwa kufanyika Juni 29 mwaka huu baada ya tarehe iliyokuwa imepangwa awali Mei 3 mwaka huu kupanguliwa baada ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Michezo na Klabu kukataa kuipitisha Katiba ya klabu hiyo iliyofanyiwa marekebisho hivi karibuni.

    Akizungumza na waandishi wa habari leo makao makuu ya Simba SC zilizopo mtaa wa Msimbazi, Kariakoo jijini Dar es Salaam mchana huu, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Simba, Damas Ndumbaro amesema kamati yake iliyokutana jijini Dar es Salaam jana, imeamua uchaguzi huo ufanyike Juni 29 kupata Rais, Makamu wa Rais na wajumbe wa kamati mpya ya utendaji ya Simba."Kamati yangu ina watu makini, waadilifu na wenye mawazo chanya kwa klabu ya Simba. Mara baada ya msajili kupitisha katiba juzi, jana tulikutana mara moja kupanga ratiba ya uchaguzi. Hatutakuwa na huruma dhidi ya watu watakaokiuka kanuni za uchaguzi," amesema Ndumbaro mwenye PhD ya Sheria.

    Kuchelewa kwa uchaguzi huo kunaufanya uongozi wa sasa chini ya mwenykiti Ismail Aden Rage kuzidisha muda wake wa miaka nminne tangu Mei 10, 2010 unaolizika Mei 10 mwaka huu, Jumamosi ijayo.

    RATIBA YA MCHAKATO UCHAGUZI SIMBA SC

    Mei 9, 2014: Kwanzaa kutoa fomu
    Mei 14, 2014: Kurudisha fomu 
    Mei 17, 2014: Uhakiki wa fomu za wagombea 
    Mei 19, 2014: Kutangaza majina ya wagombea 
    Mei 20, 2014: Kupokea pingamizi dhidi ya wagombea 
    Mei 25, 2014: Kusikiliza pingamizi 
    Mei 27, 2014: Usaili wa wagombea 
    Mei 29, 2014: Kutangaza matokeo ya usaili 
    Mei 30, 2014: Masula ya kimaadili 
    Juni 2-9, 2014: Kukata rufaa kamati ya rufaa 
    Juni 2-7, 2014: Maamuzi ya kamati ya maadili 
    Juni 10-12, 2014: Kusikiliza rufaa Juni 8-12
    Juni 16, 2014: Kukata rufaa kamati ya rufaa ya maadili 
    Juni 16-20, 2014: Maamuzi ya mwisho ya kamati ya rufaa na kamati ya rufaa ya maadili
    Juni 21-23, 2014: Kutangaza orodha ya mwisho ya wagombea 
    Juni 24-28, 2014: Kampeni 
    Juni 29, 2014: Uchaguzi mkuu
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA SC UCHAGUZI JUNI 29 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top