TIMU ya Hispania imefanikiwa kutinga Fainali ya Kombe la Dunia baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Ufaransa usiku huu Uwanja wa AT&T Jijini Arlington, in Tarrant County, Texas nchini Marekani.
Mabao ya La Roja yamefungwa na mshambuliaji wa Real Sociedad ya kwao, Hispania, Mikel Oyarzabal Ugarte dakika ya 22 kwa penalti na beki wa kulia wa club Tottenham Hotspur ya England, Pedro Antonio Porro Sauceda dakika ya 58.
Sasa Hispania watamsubiri mshindi wa Nusu Fainali ya pili kati ya mabingwa watetezi, Argentina na England zitakazomenyana baadaye leo Uwanja wa Mercedes-Benz Jijini Atlanta Georgia, Marekani.
Fainali ya Kombe la Dunia 2026 itapigwa Julai 19 Uwanja wa MetLife Jijini East Rutherford, in Bergen County, New Jersey nchini Marekani ikitanguliwa na mechi ya kusaka mshindi wa tatu, Julai 18 Uwanja wa Hard Rock, Miami Gardens, Florida, Marekani.



.png)
0 comments:
Post a Comment