TIMU ya Ufaransa imefanikiwa kwenda Nusu Fainali ya Kombe la Dunia baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Morocco katika mchezo wa Robo Fainali usiku wa kuamkia leo Uwanja wa Gillette Jijini Foxborough, Norfolk County, Massachusetts, Marekani.
Mabao yote ya Ufaransa yamefungwa na washambuliaji wake wenye asili ya Afrika, Kylian Mbappé Lottin wa Real Madrid ya Hispania mwenye asili ya Cameroon dakika ya 60 na Masour Ousmane Dembélé wa Paris Saint-Germain ya Kwai, Paris mwenye asili ya Mauritania, Senegal na Mali dakika ya 66.
Ufaransa wanders kuondoka na ushindi mnene zaidi kama Nahodha wake, Mbappe asingekosa penalti dakika ya 28, ambayo iliokolewa na kipa wa Al Hilal ya Saudi Arabia, Yassine Bounou mzaliwa wa Canada.
Sasa Ufaransa itakutana na mshindi wa Robo Fainali ya pili kati ya Hispania na Ubelgiji zitakazomenyana leo Uwanja wa SoFi, Inglewood, Kusini-Magharibi mwa Los Angeles, California, Marekani.



.png)
0 comments:
Post a Comment