TIMU ya Ubelgiji imetoa sare ya kufungana bao 1-1 na Misri katika mchezo wa Kundi G Fainali za Kombe la Dunia usiku huu Uwanja wa Lumen Field Jijini Seattle, Washington, Marekani.
Kiungo Emam Ashour Metwally Abdel Ghany alianza kuifungia Misri dakika ya 19, kabla ya mchezaji mwenzake wa Al Ahly ya nyumbani, Cairo – beki Mohamed Hany Gamal El-Demerdash kujifunga dakika ya 66 katika jitihada za kuokoa na kujiikuta anaipatia Ubelgiji bao la kusawazisha.
Mchezo mwingine wa Kundi G utafuatia baadaye kati ya Iran na New Zealand Uwanja wa SoFi Jijini Inglewood, Los Angeles, California, Marekani.



.png)
0 comments:
Post a Comment