Suleiman Kidunda, mmoja wa mabondia nyota Tanzania, hapa akiwa rais Jakaya Kikwete, naye anatarajiwa kushiriki mashindano ya taifa |
Na Prince Akbar
SHIRIKISHO
la Ngumi Tanzania (BFT)limeandaa mashindano ya ngumi ya ubingwa wa Taifa,
yatakayofanyika kuanzia Septemba 17 hadi 22, mwaka huu, Uwanja wa ndani wa Taifa,
kila siku kuanzia saa 9.00 alasiri.
Rais wa BFT,
Makore Mashaga ameiambia BIN ZUBEIRY kwamba Awali mashindano
hayo yalikuwa yamepangwa kufanyika kuanzia Septemba 15, lakini kutokana na Uwanja
wa Ndani wa Taifa kuwa na shughuli nyingine ya kimichezo, Ligi ya mpira wa
kikapu, sasa mashindano hayo yataanza kutimua vumbi siku mbili mbele zaidi.
Amesema lengo
la mashindano hayo ni kupata timu ya taifa ya ngumi yenye sura ya kitaifa, itakayoshirikisha
mikoa yote ya Tanzania Bara, ili kuanza maandalizi ya mapema na ya uhakika kwa
ajili ya kushiriki mashindano ya Jumuiya ya Madola 2014, mashindano ya Afrika
2015, mashindano ya Olimpiki 2016, ubingwa wa dunia na mashindano mengine mbalimbali.
Amesema hadi
sasa, jumla ya mikoa 18 imethibitisha kushiriki mashindano hayo, ambayo ni
Temeke, Kinondoni, Ilala, Ngome ya JWTZ, JKT, Magereza, Polisi, Pwani, Morogoro,
Mbeya, Ruvuma, Dodoma, Kigoma, Kagera, Tanga, Arusha, Tabora na Mwanza.
Amesema BFT
licha ya kutopata udhamini wa uhakika wa kufanikisha mashindano haya, kwa
kushirikiana na wadau mbalimbali umejipanga vema kuhakikisha mashindano hayo yanafanyika
kwa kiwango cha hali ya juu ili kufikia lengo la kupata timu ya taifa kwa
wakati kwa maandalizi ya mapema.
Amesema
jumla ya Sh. Milioni 26 zinahitajika kufanikisha mashindano hayo.
0 comments:
Post a Comment