Shujaa wa Yanga SC leo ni mlindamlango, Abdultwalib Mshery aliyeokoa penalti ya beki wa kati raia wa Ivory Coast, Ahoutou Angenor Landry Zouzou.
Waliofunga penalti za Yanga ni washambuliaji Emmanuel Mwanengo, Mzimbabwe Prince Dube, viungo Pacome Zouzoua, Mudathir Yahya na beki na Nahodha, Bakari Nondo Mwamnyeto.
Waliofunga penalti za Azam FC ni kiungo, Yahya Zayd, beki Twalib Nuru, kiungo raia wa Mali, Sadio Kanoute na mshambuliaji Ngita Kamanya.

Yanga ingeweza kuondoka na ushindi mapema tu kama kiungo wake Muivory Coast, Peodoh Pacome Zouzoua amgefunga penalti dakika ya 115, lakini ikaokolewa na kipa Aishi Salum Manula.
Aidha, Yanga SC pia ilishindwa kutumia mwanya wa Azam FC kucheza pungufu tangu dakika ya 55 baada ya winga wa Kimataifa wa Mali, Cheickna Diakité kutolewa kwa kadi nyekundu kufuatia kuonyeshwa kadi ya pili ya njano.
Nyota kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) waliibuka vinara wa michuano hiyo – kiungo wa Yanga SC, Maxi Mpia Nzengeli akiwa Mchezaji Bora na mshambuliaji wa Azam FC, Jephte Kitambala Bola akiwa Mfungaji Bora kwa mabao yake mawili, Aishi Manula Kipa Bora, kiungo mshambuliaji chipukizi Kelvin Arbogast Kiobya (17) akiwa Mchezaji Bora Chipukizi.



.png)
0 comments:
Post a Comment