• HABARI MPYA

    Saturday, January 10, 2026

    RAIS DK SAMIA AWAALIKA IKULU TAIFA STARS KWA PONGEZI ZA 16 BORA AFCON


    RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan ameipongeza timu ya taifa ya sika ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kwa kufika Hatua ya 16 Bora Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 nchini Morocco.
    Katika hafla maalum ya kuwapongeza wanamichezo na timu
    zilizofanya vizuri kwenye michezo ya Kimataifa iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam mapema leo, Nahodha wa Taifa Stars, Bakari Nondo Mwamnyeto amemzawadia jezi Rais Dk. Samia iliyosainiwa na wachezaji wenzake wote kama ishara ya kutambua mchango wake kwenye sekta ya michezo.



    Safari ya Tanzania katika Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 iliishia Hatua ya 16 Bora baada ya kutolewa na wenyeji, Morocco Jumapili ya Januari 4 kufuatia kufungwa 1-0 Uwanja wa Prince Moulay Abdellah Jijini Rabat.
    Bao pekee la Simba wa Atlasi lililoiangusha Taifa Stars lilifungwa na winga wa Real Madrid ya Hispania, Brahim Abdelkader Díaz dakika ya 64.
    Lakini siku hiyo Kocha wa Tanzania, Muargentina Miguel Angel Gamondi na wachezaji wake walimlalamikia refa Boubou Traore wa Mali kuwanyima penalti kufuatia winga Iddi Suleiman ‘Nado’ kuangushwa kwenye boksi dakika ya 90 na ushei.
    Rais Samia pia amempongeza Mwanariadha Alphonce Felix Simbu kwa kutwaa Medali ya Dhahabu kwenye mashindano ya Dunia mwaka jana.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RAIS DK SAMIA AWAALIKA IKULU TAIFA STARS KWA PONGEZI ZA 16 BORA AFCON Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top