• HABARI MPYA

    Wednesday, January 14, 2026

    MANE AIPELEKA SENEGAL FAINALI AFCON


    TIMU ya Senegal imefanikiwa kwenda Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Misri usiku huu Uwanja wa Tangier Grand Jijini Tangier nchini Morocco.
    Bao pekee la Simba wa Teranga katika mchezo huo mtamu wa Nusu-Fainali AFCON 2025 limefumgwa na mshambuliaji wa zamani wa Liverpool, Sadio Mané ambaye kwa sasa anachezea Al-Nassr ya Saudi Arabia dakika ya 78.
    Senegal sasa itakutana na mshindi wa Nusu Fainali ya pili kati ya wenyeji, Morocco na Nigeria watakaomenyana kuanzia Saa 5:00 usiku Uwanja wa Prince Moulay Abdellah Jijini Rabat.
    Nyota wa Liverpool, Mohamed Salah na wa Manchester City, Omar Marmoush hawakuweza kuwasaidia Mafarao kufurukuta mbele ya Simba wa Teranga. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MANE AIPELEKA SENEGAL FAINALI AFCON Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top