• HABARI MPYA

    Thursday, July 12, 2012

    SIMBA NA URA SASA JUMAPILI TAIFA KAGAME


    Musonye kulia, kushoto ni Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah


    Na Prince Akbar
    BARAZA la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) limerekebisha ratiba ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame na sasa mabingwa wa Tanzania, Simba SC watacheza na URA Jumapili, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, badala ya Jumatatu.
    Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholaus Musonye ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba, mechi ya Simba imerudishwa Jumapili, baada ya fainali ya Copa Coca Cola kuhamishiwa Uwanja wa Karume siku hiyo, tofauti na awali ilipangwa kufanyika Uwanja wa Taifa hivyo kusababisha mechi ya Simba na URA isogezwe mbele.
    Kwa mabadiliko hayo, sasa Jumapili kutakuwa kuna mechi tatu za Kagame, mechi ya Simba na URA Uwanja wa Taifa itatanguliwa na mechi kati ya Vita Club ya DRC na Ports ya Djibouti, wakati Chamazi Azam itamenyana na Mafunzo ya Zanzibar.  

    RATIBA KOMBE LA KAGAME:
    Julai 14, 2002
    1 APR vs WAU SALAAM Uwanja wa Taifa (Saa 8 mchana)
    2 YANGA vs ATLETICO Uwanja wa Taifa (saa 10 jioni)

    Julai 15, 2002
    3 AZAM vs MAFUNZO Chamazi (saa 8 mchana)
    4 VITA CLUB vs PORTS Uwanja wa Taifa (saa 10 jioni)
    5 SIMBA vs URA Uwanja wa Taifa (saa 10 jioni)

    Julai 17, 2012
    6 ATLETICO vs APR Uwanja wa Taifa (saa 8 mchana)
    7 WAU SALAAM vs YANGA Uwanja wa Taifa (saa 10 jioni)
    Julai 18, 2012
    8 VITA CLUB vs URA Uwanja wa Taifa (saa 8 mchana)
    9 PORTS vs SIMBA Uwanja wa Taifa (saa 10jioni)
    Julai 19, 2012
    10 ATLETICO vs WAU SALAAM Uwanja wa Taifa (saa 8 mchana)
    11 MAFUNZO vs TUSKER Uwanja wa Taifa (saa 10 jioni)

    Julai 20, 2002
    12 PORTS vs URA Uwanja wa Taifa (saa 8 mchana)
    13 YANGA vs APR Uwanja wa Taifa (saa 10 jioni)

    Julai 21, 2012
    14 AZAM vs TUSKER Uwanja wa Taifa (saa 8 mchana)
    15 SIMBA vs VITA CLUB Uwanja wa Taifa (saa 10 jioni)

    Julai 22m, 2012 (MAPUMZIKO)

    ROBO FAINALI
    Julai 23, 2012
    16 B2 vs C2
    17 A1 vs C3

    Julai 24, July
    18 C1 vs A2
    19 B1 vs A3

    Julai 25, 2012 (MAPUMZIKO)

    NUSU FAINALI
    Julai 26, July
    20 Winner 16 vs Winner 17
    Julai 26, 2012
    21 Winner 18 vs Winner 19

    Julai 27, 2012 (MAPUMZIKO)

    FAINALI NA MSHINDI WA TATU
    Julai 28, 2012
    22 Loser 20 vs Loser 21
    23 Winner 20 vs Winner 21
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA NA URA SASA JUMAPILI TAIFA KAGAME Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top