• HABARI MPYA

    Thursday, September 20, 2018

    RONALDO ALIMWA KADI NYEKUNDU JUVENTUS IKISHINDA 2-0 HISPANIA

    Mshambuliaji wa Juventus Cristiano Ronaldo akisikitika baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu usiku wa Jumatano kufuatia kugombana na Jeison Murillo wa Juventus wakati wa mchezo wa Kundi H Ligi ya Mabingwa Ulaya Uwanja wa Mestalla. Juventus imeshinda 2-0, mabao yote akifunga kiungo wa kimataifa wa Bosnia & Herzegovina, Miralem Pjanić na yote kwa penalti dakika za 45 na 51 na kilichomponza Ronaldo ni kwenda kumrudishia Murillo akiwa hana mpira baada ya kuchezewa rafu kwenye boksi na beki huyo Mcolombia. Hiyo ni kadi nyekundu ya 11 kwa Ronaldo kihistoria kwenye soka, lakini ya kwanza kwenye Ligi ya Mabingwa 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RONALDO ALIMWA KADI NYEKUNDU JUVENTUS IKISHINDA 2-0 HISPANIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top