• HABARI MPYA

    Wednesday, April 01, 2026

    DRC YAFUZU KOMBE LA DUNIA BAADA YA KUICHAPA JAMAICA 1-0


    TIMU ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) imefuzu Fainali za Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza baada ya miaka kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Jamaica kwenye mechi ya Mchujo wa Mabara Uwanja wa Guadalajara nchini Mexico.
    Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, beki wa Burnley ya England, Axel Tuanzebe katika dakika za ziada.
    Kabla ya mchezo huo, Tuanzebe alikaririwa akisema kwamba mchezo huo ulikuwa mkubwa zaidi katika historia yake na mchezaji huyo wa zamani wa timu ya taifa wa vijana wa England, ambaye alizaliwa Bunia, jiji lililoathiriwa na mzozo unaoendelea mashariki mwa DRC, sasa ameandika jina lake katika historia ya soka ya Kongo.
    Ingawa mshambuliaji wa Leopards Cedric Bakambu alifunga mara mbili kwa usahihi, lakini mabao yote yalikataliwa kwa kuwa alikuwa ameotea kabla na haikuwa ajanu kwamba mchezo mgumu ulihitaji dakika 30 za ziada ili kutatua mambo.
    Na ilikuwa Tuanzebe ambaye alikuwa katika nafasi sahihi kwa wakati unaofaa, akitumia mwili wake karibu kutupia mpira golini baada ya kona ya Brian Cipenga kumgonga mlinzi wa Jamaica Joel Latibeaudiere na kumkuta mchezaji huyo wa Burnley aliyekimbia kwa kasi katika dakika ya 100 na kufunga.
    Sherehe zilisitishwa kwa muda huku maafisa wakiangalia kama kuna uwezekano wa mpira kuchezwa kwa mkono, lakini VAR hatimaye iliamua kwamba mpira haukumgusa Tuanzebe mkononi.
    Jamaica, ambao walikuwa na matumaini ya kufika Kombe la Dunia kwa mara ya pili baada ya 1998 nchini Ufaransa ndoto zao zimekuwa za alinacha.
    Badala yake, ni DRC ambayo inafuzu kwa mara ya pili nayo na baada ya mwaka 1974 nchini Ujerumani, wakati huo Ujerumani Magharibi.
    DRC inayofanya Afrika iwe na timu 10 sasa inakwenda moja kwa moja kuingia Kundi K ikiungana na Ureno, Colombia na Uzbekistan. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: DRC YAFUZU KOMBE LA DUNIA BAADA YA KUICHAPA JAMAICA 1-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top