• HABARI MPYA

    Sunday, April 05, 2026

    AZAM FC NA SIMBA SC HAKUNA MBABE, ZATOKA SULUHU CHAMAZI


    TIMU za Azam FC na Simba SC zimetoshana nguvu kwa sare ya bila mabao katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Jijini Dar es Salaam.
    Ulikuwa mchezo mzuri wa kiufundi na maarifa, timu zote — Azam FC inayofundishwa na Kocha Mkongo Jean-Florent Ikwange Ibenge na Simba SC ya Kocha raia wa Afrika Kusini, Steven Robert Barker zikishambuliana kwa zamu.
    Kwa matokeo hayo, Azam FC inafikisha pointi 33 katika mchezo wa 17, ingawa inabaki nafasi ya tatu ikizidwa pointi mbili na Simba SC ambayo pia ina mechi moja mkononi.
    Ikumbukwe, mabingwa watetezi, Yanga SC ndio wanaongoza Ligi Kuu kwa pointi zao 41 za mechi 17.
    Next
    This is the most recent post.
    Older Post
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC NA SIMBA SC HAKUNA MBABE, ZATOKA SULUHU CHAMAZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top