TIMU ya TRA United imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Singida Black Stars katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini Arusha.
Mabao ya TRA United yote yamefungwa na mabeki, mzawa Abdallah Kheri ‘Ssebo’ aliyejifunga dakika ya 10 na Mganda Christopher Tebandeke kwa penalti dakika ya 40.
Kwa ushindi huo, TRA United inafikisha pointi 23 katika mchezo wa 17 ikisogea nafasi ya nane kutoka ya 10, wakati Singida Black Stars inabaki na pointi zake 25 za mechi 17 sasa ikisalia nafasi ya sita.
Baada ya mchezo huo, Singida Black Stars imetangaza kuondoa Maafisa wote wa benchi lake la Ufundi kutokana na mfululizo wa matokeo mabaya.




.png)
0 comments:
Post a Comment