• HABARI MPYA

    Thursday, March 26, 2026

    TAIFA STARS YACHAPWA 1-0 NA LIECHTENSTEIN MICHUANO YA FIFA SERIES KIGALI


    TANZANIA imefungwa bao 1-0 na Liechtenstein katika mchezo wa Nusu Fainali ya Kundi B michuano ya FIFA Series jioni ya leo Uwanja wa Pele Jijini Kigali nchini Rwanda.
    Bao pekee la Liechtenstein limefungwa na winga, Ferhat Sağlam
    wa Eintracht Hohkeppel inayoshiriki Ligi ya Ridhaa Daraja la Tano Ujerumani ijulikanayo kama Mittelrheinliga dakika ya 56.
    Mapema katika mchezo uliotangulia mchana Aruba iliichapa Macau 4-1 hapo hapo Uwanja wa Pele Jijini Kigali.
    Sasa Taifa Stars itakamilisha michuano hiyo Jumapili kwa kucheza na Macau Jumapili kuwania nafasi ya tatu ya kundi lake, wakati Liechtenstein itamenyana na Aruba katika Fainali kwa Kundi B. 
    Next
    This is the most recent post.
    Older Post
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TAIFA STARS YACHAPWA 1-0 NA LIECHTENSTEIN MICHUANO YA FIFA SERIES KIGALI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top