• HABARI MPYA

    Sunday, May 17, 2026

    NI USM ALGER MABINGWA WA KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA


    TIMU ya USM Alger ya Algeria imefanikiwa kutwaa Kombe la Shirikisho Afrika baada ya ushindi wa Penalti 8-7 dhidi ya wenyeji, Zamalek kufuatia sare ya jumla ya 1-1 usiku wa jana Uwanja wa Cairo International Jijini Cairo nchini Misri.
    Zamalek walifanikiwa kumaliza dakika 120 za jana wakiwa wameshinda 1-0, bao la mshambulijai wa Kimataifa wa Palestina, Oday Ibrahim Mohammad Dabbagh dakika ya tano kwa penalti.
    Matokeo yakafanya sare ya jumla ya 1-1 kufuatia USM Alger nao kushinda 1-0 kwenye mchezo wa kwanza Mei 9, bao la winga Mualgeria Ahmed Khaldi kwa penalty pia dakika ya 90’+8 Uwanja wa Julai 5 Jijini Algiers.
    Aliyewapa taji hilo USM Alger ni kiungo Mmisri, Mohamed Shehata Mahmoud aliyepiga juu ya lango mkwaju wake wa penalty na kuhitimisha kazi kwa kuikosesha Zamalek taji nyumbani.
    Miongoni mwa waliofunga penalty zao jana ni Abdullah El-Said, Hossam Abdel-Maguid, Seif El-Jaziri na Mbrazil Juan Bezerra upande wa Zamalek, wakati Ahmed Khaldi, Zakaria Draoui, Saad Radouani na Ben Ayad waliifungia USM.
    Hilo linakuwa taji la pili la Kombe la Kombe la Shirikisho kwa USM Alger baada ya 2023 walipoipiku Yanga ya Tanzania kwa mabao ya ugenini kufuatia sare ya jumla ya 2-2, wakishinda 2-1 Dar es Salaam na kufungwa 1-0 Algiers kwenye Fainali. 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NI USM ALGER MABINGWA WA KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top