• HABARI MPYA

    Friday, March 28, 2025

    KAGERA SUGAR YATINGA ROBO FAINALI KOMBE LA CRDB


    TIMU ya Kagera Sugar imefanikiwa kutinga Hatua ya Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano inayodhaminiwa na Benki ya CRDB baada ya ushindi wa penalti 5-3 dhidi ya wenyeji, Tabora United kufuatia sare ya 1-1 Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.
    Katika dakika 90 za mchezo huo, Tabora United ilitangulia kwa bao la beki wake Mkongo, Andy Bikoko dakika ya tatu, kabla ya kiungo mzawa, Joseph Mahundi kuisawazishia Kagera Sugar dakika ya 28.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KAGERA SUGAR YATINGA ROBO FAINALI KOMBE LA CRDB Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top