• HABARI MPYA

    Thursday, July 23, 2009

    NAKUPA LYRICS ZA MTU MZIMA SUGU...





    WIMBO: Ringa:
    MWIMBAJI: Sugu. Feat, Ngwair, Dr Levy

    NGWAIR:
    Uuuuh,Yeah, Suguu Ngwaur na Dr Levy collabo iko heavy,
    yeah,Mj... I can hear u, sex mama ringa baby, yeah!
    mtoto una rangi ya mvuto safi na pozi, vyako vito,
    vinashaini off coz, true! mtoto matawi ya juu,
    uzuri unao figa unayo usijali we ringa tuu,
    mtoto unang'aa gheto mwanga wa mshumaa,
    nipe zidi ya catwalk unapokrosi kwa mtaa,
    ah, ah, uzuri wako wa asili akili wako utajiri
    heshima hadi usafiri kuringa unastahili (ringaa),
    bambataa utadhani mko wawili,
    siyo siri wengi tu unawachanganya akili, (ringaa),
    wala usione soo, kwani tayari tupo kwenye dancing floor,
    so deep it low then bring it up slow,
    unapokata machizi wote wanabaki like woo!
    ha, haa, ringa tuu mamaa we kifaa japo wazushi bado wanakataa,
    we ringaa...

    CHORUS:
    Ringa ringa ringa ringa kama unavyoringaa..
    (ringaa) ringa ringa ringa baby kama unavyoringagaa...
    ( we ringaa) x 2


    DR LEVY:
    Hahaaaa! uuuh!mtoto umeumbika maridadi unanipa midadi,
    ah sikusifii makusudi una thamani zaidi ya gold,
    Bongo ingejivunia kama ungekuwa first lady,
    siyo tu nakusifia ukweli nakwambia mamaa,
    kuwa nawe binafsi najivunia, umbo lako ni la ajabu,
    halijifichi hata unapovaa hijabu,
    kama ungependa umiss ungeshinda,
    hakuna jaji wa kupinga miss world usingedunda,
    ah, ungetoa nuksi kwa mtu mzima Lundenga,
    kama kawaida hupandishi mitungi kinywaji chako ni soda,
    unang'ara bila poda baby, na kwa upeo mtoto mi nakupa shada,
    kukumiliki ni zali nasema asante mungu,
    hata shule hukufeli na unaishi kiswahili,
    hupendi kabisa uzungu, ah, kwangu fahari,
    we ni binti mrembo, sita kwa sita mtoto unayajua mambo,
    sitaki tena shombo sitaleta mtoto wa kambo,
    naogopa kukupa mimba ntatibua shepu ya tumbo,
    japo kuzaa ni lazima na nataka ubaki kama pambo,
    kuna watu wanachonga eti mtoto unaringa nami siwezi kupinga
    nasema ruksa kuringa... wooo.

    CHORUS:
    Ringa ringa ringa ringa kama unavyoringaa..
    (ringaa) ringa ringa ringa baby kama unavyoringagaa...
    ( we ringaa) x 2

    SUGU:
    Nimeshaona mademu kutoka kila sehemu,
    una haki ya kuringa we ni bonge la demu,
    mtaani ni nani asiyekufahamu,
    kila time nikikuona usoni unatabasamu,
    machoni kukutazama mtu mzima siishi hamu,
    una maumbile matamu, na zaidi umetulia
    na kichwani uko timamu,
    ha, na huna mzuka wa kutaka kwenda Ulaya,
    unakomaa na chuo ili baadaye uwe lawyer,
    wewe siyo sister duu kanyaboya,
    uzuri kama wako wengine wanautumia kwa umalaya,
    napenda hata mavazi unayovaa,
    napenda pozi zako kwenye kiti unapokaa,
    ukisimama tumbo flati utadhani bado hujazaa,
    ha, nje kimini lazima thong kwa ndani,
    na gitaa la nyuzi kadhaa kiunoni,
    na ndo maana nikiwa nawe mkono daima uko ndani,
    na ukienda club mabitozi ni vurugu lakini wanatulia
    wanapojua uko na Sugu, kwani wanajua Sugu pia ni mtu wa mavurugu...
    ringaa ringaa...

    CHORUS: Ringa ringa ringa ringa kama unavyoringaa..
    (ringaa) ringa ringa ringa baby kama unavyoringagaa...
    ( we ringaa) x 2






    WIMBO: Kiburi
    MWIMBAJI: Sugu Feat. Stara Stara:

    STARA:
    Wanachotaka wewe upate tabu
    Raha kidogo tu chuki bila sababu
    SUGU: Najua mama, hili ntalikabili,
    Kwani najua jeuri dawa yake ni kiburi

    VESI LA KWANZA
    Kwa wanaonijua toka enzi za Mbeya Day,
    au wakati bado mdogo mama aliponiita May,
    miaka chini ya kumi tu nina jina mtaani,
    kila mtu alinijua mimi mtoto wa nani,
    ni hivyo hivyo mpaka waalimu shuleni,
    na ndo maana mpaka leo mimi sishangai kushaini,
    nilipoanza muziki sikujua mafanikio yangeambatana na chuki
    mara ngapi nageukwa na nnaowaita marafiki?
    sasa nalala macho wanafiki siwataki,
    maana kila ninachofanya wanaonekana hawataki,
    Ha! na sijali wanachosema,
    Baba alinifundisha kutazama mbele daima,
    na moto ni ule ule tu hakuna wa kuuzima,
    najua wanachotaka, kuona Sugu kachoka…
    …ili wapate kucheka, watasubiri watachoka,
    watapanda watashuka, mi nabaki vile vile kila siku kila mwaka,
    na bado wanakilisha tu chama la Madeiwaka,
    mi ni fighter nafaiti bila kuchoka...
    aaaaaaaaaah aaaaaaaaaaaaaaah!

    STARA:
    Wanachotakaaa ooh wanavyotaka...
    Wanachotaka wewe upate tabu
    Raha kidogo tu chuki bila sababu


    VESI LA PILI:
    Kweli jeuri dawa yake ni kiburi,
    na mi ntabaki mbishi mpaka nilione kaburi,
    wako wapi walionicheka shuleni nilipofeli,
    pilika zangu mtaani zimenifikisha mbali,
    tisini na tatu niko boda naitafuta South Afrika,
    leo kila nnapotaka naenda zangu Amerika,
    ndivyo maisha yanavyoweza kuchenji,
    leo niko na Terrano kesho VX au Range,
    na bado nikiwa Bar nadai chenji, Ha,
    pata picha Sugu angekuwa kisha choka,
    hakika historia ingekuwa imeshafutika,
    mabwana mdogo wangeongea kuhusu gemu wanavyotaka,
    ningetoweka kama wastaafu wa soka,
    kumbuka niliacha fani wakasema wananimiss,
    nimerudi kwa kishindo wengine wanapata stress,
    wanabaki tu wanasema... na, mi nasema waseme watakavyosema,
    kwani watasema mchana na usiku watalala,
    na wakiamka asubuhi mi naendeleza bakora, waah!

    STARA:
    Wanachotaka wewe upate tabu
    Raha kidogo tu chuki bila sababu

    VESI LA TATU
    Maisha yangu yote nimepata sana tabu,
    nashangaa raha kidogo tu chuki bila sababu,
    sijawafanyia madhambi vipi wanataka nitubu?!
    wanasema nikisema wanasema mi nna gubu,
    najua bado niko juu kwenye listi,
    sina mchezo na life ila siogopi kulosti,
    haya siyo maisha yangu nyie mafala,
    yote ni mambo tu ya hela,
    siku nikikosa mchuma niko ndani ya daladala,
    na hata kama ni kweli mi sikuzaliwa gheto,
    nimekulia street na nimeshazoea msoto,
    na enzi zangu machizi waliniita msela ngoto,
    na kwa Madj sitoi rushwa za kitoto,
    hata waendelee kubana hawatazuia ndoto,
    au niende PCB niwapelekee za moto?
    kama noma iwe noma na ikibidi ile kinoma,
    wananiua kimuziki kwa nini nione huruma?

    STARA:
    Wanachotaka wewe upate tabu
    Raha kidogo tu chuki bila sababu
    Wanachotaka wewe upate tabu, raha kidogo tu chuki bila sababu,

    SUGU: Najua mama hili ntalikabili kwani najua jeuri dawa yake ni kiburi
    STARA: Wanachotaka wewee upate tabu raha kidogo tu chuki bila sababuAh!
    SUGU: Najua mama, hili ntalikabili kwa najua jeuri dawa yake ni kiburi haaa!
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NAKUPA LYRICS ZA MTU MZIMA SUGU... Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top