• HABARI MPYA

    Sunday, December 07, 2025

    YANGA SC YAICHAPA COASTAL UNION 1-0 DODOMA


    MABINGWA watetezi, Yanga SC wameibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara usiku huu Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.
    Haukuwa ushindi mwepesi, kwani iliwalazimu Yanga kusubiri hadi dakika tatu za mwisho pale mshambuliaji wake tegemeo, Mzimbabwe Prince Dube Mpumelelo alipounganisha kwa kichwa krosi ya kiungo Muivory Coast dakika ya 87 kufunga bao hilo pekee.
    Kwa ushindi huo, timu ya Wananchi inafikisha pointi 16 katika mchezo wa sita na kusogea nafasi ya pili, wakati Coastal Union inabaki na pointi zake tisa za mechi nane sasa nafasi ya 11.

    Next
    This is the most recent post.
    Older Post
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA SC YAICHAPA COASTAL UNION 1-0 DODOMA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top