• HABARI MPYA

    Friday, December 26, 2025

    ANGOLA NA ZIMBABWE ZAGAWANA POINTI KWA SARE YA 1-1 AFCON


    TIMU za Angola na Zimbabwe zimetoka sare ya kufungana bao 1-1 jioni hii katika mchezo wa Kundi B Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 Uwanja wa Marrakech Jijini Marrakech nchini Morocco.
    Mshambuliaji wa Al-Wakrah ya Qatar, Jacinto Muondo ‘Gelson’ Dala alianza kuifungia Palancas Negras dakika ya 24, kabla ya mshambuliaji wa Scottland FC ya kwao, kuisawazishia The Warriors dakika ya 45’+6.
    Kwa matokeo hayo, kila timu inaokota pointi ya kwanza baada ya wote kupoteza mechi zao za kwanza, Angola ikifungwa 2-1 na Afrika Kusini na Zimbabwe ikichapwa 3-1 na Misri.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ANGOLA NA ZIMBABWE ZAGAWANA POINTI KWA SARE YA 1-1 AFCON Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top