• HABARI MPYA

    Monday, December 29, 2025

    YANGA SC YAMSAJILI MCHEZAJI WA TRA UNITED


    KLABU ya Yanga imemtambulisha mshambuliaji chipukizi, Emmanuel Samuel Mwanengo (22) kuwa mchezaji wake mpya akijiunga na timu hiyo kutoka TRA United ya Tabora.
    Mwanengo aliibukia Nyangobo FC ya Zanzibar kabla ya kwenda Tajikistan mwaka 2023 ambako alichezea Ravshan Kulob na Vakhsh mwaka 2024, kabla ya kurejea nchini mwaka huu kujiunga na TRA United, zamani Tabora United.
    Na baada ya kuonyesha uwezo wake katika Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara ndani ya Nusu msimu anahamia kwa Wananchi kuendeleza kampeni ya kushinda mataji.
    Next
    This is the most recent post.
    Older Post
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA SC YAMSAJILI MCHEZAJI WA TRA UNITED Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top