TUNISIA imeanza vyema Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Uganda usiku wa kuamkia leo katika mchezo wa Kundi C Uwanja wa Olimpiki Jijini Rabat nchini Morocco.
Mabao ya Eagles of Carthage yamefungwa na viungo, Ellyes Joris Skhiri wa Eintracht Frankfurt ya Ujerumani dakika ya 10 na Mohamed Elias Achouri wa FC Copenhagen ya Denmark mawili dakika ya 40 na 64, wakati la The Cranes lilifungwa na mshambuliaji wa APR ya Rwanda, Denis Omedi dakika ya 90’+2.
Ikumbukwe mechi ya kwanza ya Kundi C jana Nigeria iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Tanzania Uwanja wa Fez mjini Fez nchini Morocco.
Mabao ya Super Eagles yalifungwa na beki wa Hull City ya England, Oluwasemilogo Adesewo Ibidapo "Semi" Ajayi dakika ya 36 na winga wa Atalanta ya Italia, Ademola Lookman Olajade Alade Ayoola Lookman dakika ya 52, wakati la Taifa Stars limefungwa na kiungo wa Floriana ya Malta, Kokola Charles William M'Mombwa dakika ya 50.
Ikumbukwe mechi ya kwanza ya Kundi C jana Nigeria iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Tanzania Uwanja wa Fez mjini Fez nchini Morocco.
Mabao ya Super Eagles yalifungwa na beki wa Hull City ya England, Oluwasemilogo Adesewo Ibidapo "Semi" Ajayi dakika ya 36 na winga wa Atalanta ya Italia, Ademola Lookman Olajade Alade Ayoola Lookman dakika ya 52, wakati la Taifa Stars limefungwa na kiungo wa Floriana ya Malta, Kokola Charles William M'Mombwa dakika ya 50.



.png)
0 comments:
Post a Comment