• HABARI MPYA

    Sunday, December 07, 2025

    WAVULANA WA TANZANIA WATINGA NUSU FAINALI SHULE ZA AFRIKA


    TIMU ya Wavulana ya Tanzania imefanikiwa kuingia Nusu Fainali ya Mashindano ya Ubingwa wa Shule za Afrika kanda ya CECAFA baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Sudan Kusini jiini ya leo Uwanja wa St. Mary's-Kitende, Wakiso, Barabara ya Entebbe, Uganda. 
    Kwa ushindi huo, vijana wa Tanzania chini ya Kocha Boniphace Pawasa wanamaliza hatua ya awali na pointi nne kufuatia jana kuchapwa 1-0 na Ethiopia na kutoa sare ya 0-0 na Rwanda hapo hapo Uwanja wa St. Mary's-Kitende. 
    Timu ya wasichana ya Tanzania jana ilijihakikishia tiketi ya Nusu Fainali ya Michuano hiyo ya African Schools Football Championship CECAFA Zone (ASFCCQ) baada ya kuichapa Sudan Kusini 2-1 na Djibouti 6-0 Uwanja wa FUFA Kadiba, Mengo, Rubaga Jijini Kampala nchini Kampala, Uganda.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WAVULANA WA TANZANIA WATINGA NUSU FAINALI SHULE ZA AFRIKA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top