• HABARI MPYA

    Wednesday, December 24, 2025

    BURKINA FASO YATOKA NYUMA. DAKIKA YA. 90 NA USHEI KUSHINDA 2-1


    TIMU ya Burkina Faso imeanza vyema Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 baada ya ushindi wa mabao 2–1 dhidi ya Equatorial Guinea jioni ya leo Uwanja wa Mohammed V Jijini Casablanca nchini Morocco.
    Mabao ya The Stallions yamefungwa na winga wa Seattle Sounders FC ya Marekani, Georgi Minoungou dakika ya 90’+5 na beki wa kati wa  Bayer Leverkusen ya Ujerumani, Edmond Fayçal Tapsoba dakika ya 90’+8, wakati la limefungwa na beki wa kati pia wa  SS Reyes ya Hispania, Marvin José Anieboh Pallaruelo dakika ya 85. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BURKINA FASO YATOKA NYUMA. DAKIKA YA. 90 NA USHEI KUSHINDA 2-1 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top