• HABARI MPYA

    Sunday, December 28, 2025

    SUDAN YAICHAPA EQUATORIAL GUINEA 1-0 AFCON


    TIMU ya Sudan imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Equatorial Guinea katika mchezo wa Kundi E Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 usiku huu Uwanja wa  Mohammed V Jijini Casablanca nchini Morocco.
    Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Messie Nkounkou wa Kongo-Brazzaville, bao pekee la Sudan limefungwa na beki wa Torino FC ya Italia, Saúl Basilio Coco-Bassey Oubiña mzaliwa wa Hispania aliyejifunga dakika ya 74'.
    Kwa ushindi huo, Sudan inabeba pointi tatu za kwanza katika mchezo wa pili kufuatia kufungwa 3-0 na Algeria kwenye mchezo wa kwanza.
    Kwa upande wao Equatorial Guinea wanafikisha mechi mbili za kucheza bila pointi hata moja kufuatia kufungwa 2-1 na Burkina Faso kwenye mchezo wa kwanza. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SUDAN YAICHAPA EQUATORIAL GUINEA 1-0 AFCON Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top