KLABU ya Simba SC imemtambulisha beki wa kushoto, Nickson Clement Kibabage (25) kuwa mchezaji wake mpya akijiunga na klabu hiyo kutoka Singida Black Stars.
Kibabage alijiunga tena na Singida Black Stars msimu huu akitokea Yanga alikodumu kwa misimu miwili kati ya mwaka 2023-2025.
Alikwenda Yanga SC akitokea Singida Black Stars ambako awali alicheza kwa msimu mmoja akitokea KMC ambako alikuwa anacheza kwa mkopo kutoka Difaâ Hassani El Jadidi ya Morocco.
Kibabage alijiunga na Difaâ Hassani El Jadidi mwaka 2019 akitokea Mtibwa Sugar iliyomuibua katika timu yake ya vijana na kufanya vizuri kikosi cha kwanza msimu mmoja tu, 2018-2019 kabla ya kuuzwa Morocco kwa mkataba wa miaka minne.



.png)
0 comments:
Post a Comment