• HABARI MPYA

    Friday, December 19, 2025

    AZAM FC NA SIMBA ZATENGANISHWA MAKUNDI KOMBE LA MAPINDUZI


    TIMU ya Azam FC imepangwa Kundi A katika Kombe la Mapinduzi Zanzibar pamoja na mabingwa watetezi, Mlandege SC, Singida Black Stars na URA ya Uganda.
    Katika michuano hiyo itakayoanza Desemba 28, Simba SC wamepangwa Kundi B Pamoja na Mwembe Makumbi City ya Unguja na Fufuni FC ya Pemba, wakati watani wao, Yanga wapo Kundi C pamoja na KVZ ya Unguja na TRA United ya Tabora.
    Mshindi wa kwanza na wa pili wa Kundi A watafuzu Nusu Fainali, wakati Kundi B na C ni vinara tu watasonga mbele kuwania tiketi ya Fainali.
    Mechi zote hadi za Nusu Fainali zitakazochezwa Januari 8 na 9 zitafanyika Uwanja wa New Amaan Complex, Unguja kasoro Fainali pekee itapigwa Uwanja wa Gombani, Pemba Januari 13, 2026.
    Next
    This is the most recent post.
    Older Post
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC NA SIMBA ZATENGANISHWA MAKUNDI KOMBE LA MAPINDUZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top