• HABARI MPYA

    Sunday, December 28, 2025

    AUBAMEYANG AFUNGA LAKINI GABON YACHAPWA 3-2 NA MSUMBIJI



    TIMU ya Msumbiji imeibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Gabon katika mchezo wa Kundi F Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 jioni ya leo Uwanja wa Adrar mjini Agadir nchini Morocco. 
    Mabao ya Msumbiji yamefungwa na mshambuliaji wa Mestre ya Italia, Faisal Bangal dakika ya 37, winga wa Sporting Lisbon ya Ureno, Geny Cipriano Catamo dakika ya 42 kwa penalti na beki wa kulia wa Santa Clara  ya Ureno pia, Diogo Calila dakika ya 42.
    Kwa upande wao Gabon mabao yao yamefungwa na mshambuliaji wake mkongwe na Nahodha wake, Pierre-Emerick Emiliano François Aubameyang ambaye kwa sasa anachezea Marseille ya Ufaransa dakika ya 45’+5 na beki wa kati wa Aris Limassol ya Cyprus, Alex Yowan Kevin Moucketou-Moussounda dakika ya 76.
    Kwa ushindi huo, Msumbiji inakusanya pointi tatu za kwanza katika mchezo wa pili kufuatia kuchapwa 1-0 na Ivory Coast katika mchezo wa kwanza, wakati Gabon inakamilisha mechi mbili bila hata pointi moja kufuatia kufungwa na Cameroon 1-0 pia kwenye mchezo wa kwanza.
    Baadaye Saa 5:00 usiku mechi tamu kabisa ya Kundi hilo itafuatia kati ya Tembo wa Ivory Coast na Simba Wasiofungika wa Cameroon Uwanja wa Marrakech Jijini Marrakech. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AUBAMEYANG AFUNGA LAKINI GABON YACHAPWA 3-2 NA MSUMBIJI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top