WENYEJI, Morocco wameanza vyema Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Comoro katika mchezo wa Kundi A usiku wa jana Uwanja wa Prince Moulay Abdellah Jijini Rabat.
Mabao ya Simba wa Atlasi katika mchezo huo wa ufunguzi yalifungwa na winga wa Real Madrid, Brahim Abdelkader Díaz dakika ya 55 na mshambuliaji wa Olympiacos ya Ugiriki, Ayoub El Kaabi dakika ya 74.
Morocco ingeweza kuondoka na ushindi mpana zaidi kama si kipa wa Comoro, Yannick Pandor anayedakia RC Lens ya Ufaransa kuokoa penalti ya Soufiane Rahimi dakika ya 10 tu ya mchezo huo.
Sherehe za ufunguzi zilifana zikiwahusisha Rais wa FIFA, Giannis Infantino, CAF, Dk. Patrice Motsepe na Prince Moulay Abdellah wa Morocco.
Morocco ingeweza kuondoka na ushindi mpana zaidi kama si kipa wa Comoro, Yannick Pandor anayedakia RC Lens ya Ufaransa kuokoa penalti ya Soufiane Rahimi dakika ya 10 tu ya mchezo huo.
Sherehe za ufunguzi zilifana zikiwahusisha Rais wa FIFA, Giannis Infantino, CAF, Dk. Patrice Motsepe na Prince Moulay Abdellah wa Morocco.



.png)
0 comments:
Post a Comment