• HABARI MPYA

    Wednesday, December 03, 2025

    TWIGA STARS YAKABIDHIWA MILIONI 50


    KATIBU Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo  na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa, amekabidhi Shilingi Milioni 50 kwa timu ya Taifa ya Wanawake (Twiga Stars)  kama pongezi kutoka kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kufuzu mara mbili mfululizo Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wanawake (WAFCON) 2026.
    Makabidhiano hayo yamefanyika leo Desemba 3, 2025 jijini Dar es Salaam  ikiwa ni sehemu ya Serikali kutambua  juhudi na nidhamu ya wachezaji pamoja na benchi la ufundi katika safari yao ya kufuzu michuano hiyo mikubwa  barani  Afrika, inayotarajiwa kufanyika Morocco mwaka 2026.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TWIGA STARS YAKABIDHIWA MILIONI 50 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top