• HABARI MPYA

    Monday, December 22, 2025

    DAKA AISAWAZISHIA ZAMBIA DAKIKA YA MWISHO YATOA SARE 1-1 NA MALI


    TIMU za Mali na Zambia zimetoka sare ya kufungana bao 1-1 katika mchezo wa Kundi A Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 leo Uwanja wa Mohammed V Jijini Casablanca nchini Morocco.
    Mshambuliaji wa Auxerre ya Ufaransa, Lassine Sinayoko alianza kuifungia Mali dakika ya 62, kabla ya mshambuliaji wa Leicester City yaa England, Patson Daka kuisawazishia Zambia dakika ya 90’+2.
    Kwa matokeo hayo, wenyeji Morocco wanaendelea kuongoza kufuatia ushindi wa 2-0 dhidi ya Comoro jana, wakifuatiwa na Mali na Zambia.  
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: DAKA AISAWAZISHIA ZAMBIA DAKIKA YA MWISHO YATOA SARE 1-1 NA MALI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top