• HABARI MPYA

    Saturday, May 31, 2014

    RONALDO BADO GONJWA, WASIWASI WAIKUMBA URENO

    MWANASOKA bora wa dunia, Cristiano Ronaldo alikosa mazoezi ya Ureno jana na atakosa mchezo wa kirafiki leo dhidi ya Ugiriki baada ya kulalamika maumivu ya misuli ya mguu wake wa kushoto, amesema kocha Paulo Bento jana.
    Bento hafikiri kama kutakuwa na tatizo kumkosa Ronaldo katika mchezo wa ufunguzi wa Kombe la Dunia dhidi ya Ujerumani, lakini amesema anahitaji kupona haraka kuwahi mechi zitakazofuatia.
    Ronaldo alijiunga na kikosi cha Ureno Alhamisi wiki hii pamoja na nyota wenzake wa Real Madrid, Pepe na Fabio Coentrao katika kambi ya timu yao, hoteli ya Obidos.
    Atakosekana: Cristiano Ronaldo hataichezewa Ureno katika mechi ya kirafiki dhidi ya Ugiriki leo baada ya kukosa mazoezi ya jana
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RONALDO BADO GONJWA, WASIWASI WAIKUMBA URENO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top