• HABARI MPYA

    Wednesday, May 28, 2014

    WACHEZAJI WAWILI UJERUMANI KIKOSI CHA KOMBE LA DUNIA WAPATA AJALI YA GARI

    DEREVA wa Formula One, Nico Rosberg na wachezaji wawili wa kikosi cha Ujerumani cha Kombe la Dunia wamepata ajali pamoja wakati wa kuchukua picha za promosheni katika kambi yao ya mazoezi Jumanne, ambayo ilifanya watu wawili wakimbizawe hospitali.
    Rosberg na dereva wa DTM, Pascal Wehrlein walikuwa wamewabeba wachezaji wa Ujerumani, Julian Draxler na Benedikt Howedes katika gari tofauti wakati gari la Wehrlein lilipowagonga watu wawili barabarani kaskazini mea Italiia, South Tyrol. Barabara hiyo ilikuwa imefungwa kwa matumizi ya umma.
    "Nimeshitushwa na ajali hii,"alisema Rosberg, ambaye anaongoza michuano ya ubingwa wa dunia ya Formula One baada ya kushinda Jumapoli mjini Monaco katika mbio za Grand Prix.
    Uchunguzi: Polisi wa Italia walifunga barabra hiyo baada ya ajali hiyo iloyotokea karibu na kambi ya mazoezi ya timu ya taiga ya Ujerumani mjini San Martino
    Concerns: Germany defender Benedikt Howedes was involved in the incident on Tuesday
    Brazil bound: Germany midfielder Julian Draxler plays the ball during a training session in San Martino, Italy
    Wachezaji wa kimataifa wa Ujerumani, Benedikt Howedes (kushoto) na Julian Draxler wote walihusika katika ajali

    Ujerumani imeweka kambi ya maandalizi ya Kombe la Dunia katika hotel ya Alpine kaskazini mwa Italia tangu wiki iliyopita na itaendelea kuwa huko hadi Juni 1.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WACHEZAJI WAWILI UJERUMANI KIKOSI CHA KOMBE LA DUNIA WAPATA AJALI YA GARI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top