• HABARI MPYA

    Wednesday, May 28, 2014

    NEYMAR AIJARIBU BRAZUCA, DUNIA ITAMUHESHIMU MUDA SI MREFU

    MUDA si mrefu, Neymar ataiweka dunia katika himaya yake iwapo ataiwezesha Brazil kutwaa Kombe la Dunia katika fainali zinazofanyika nyumbani kwao. 
    Na nyota huyo wa Barcelona amepata fursa ya kuujaribu mpira wa Brazuca ambao utatumika kwenye Fainali za Kombe la Dunia mwaka huu kuanzia mwezi ujao katika kambi yao ya mazoezi leo.
    Mchezaji wa Chelsea, Oscar na mchezaji mwenzake wa zamani wa timu hiyo, David Luiz walikuwa miongoni mwa wachezaji wengine walioufanyia mazoezi mpira huo leo kwa mara ya kwanza pamoja na Neymar.
    Wanaujaribu: Oscar (kushoto) na Neymar (katikati) wakiuchezea mpira wa Brazuca katika kambi yao ya mazoezi kujiandaa na fainali za Kombe la Dunia leo
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NEYMAR AIJARIBU BRAZUCA, DUNIA ITAMUHESHIMU MUDA SI MREFU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top