• HABARI MPYA

    Wednesday, May 07, 2014

    KCC WAFANYA KILE AMBACHO YANGA SC WAMESHINDWA TANZANIA

    TIMU ya Mamlaka ya Jiji la Kampala (KCCA) imefanikiwa kutetea ubingwa wa Ligi Kuu ya Shirikisho la Soka Uganda (FUFA Super League) baada ya kuichapa mabao 3-1 Sports Club Villa Uwanja wa KCCA eneo Lugogo mjini Kampala, jana.
    Kiungo wa zamani wa Yanga SC ya Tanzania, Steven Bengo alifunga bao la kwanza la KCCA dakika ya 21, kabla ya beki Ronnie Kisekka kufunga la pili dakika chache kabla ya mapumziko.
    Mabingwa; KCC wakisherehekea na taji lao
    William Wadri akafunga bao la tatu kabla ya Kiseeka kujifunga kuipatia SC Villa bao la kufutia machozi.
    Kwa ushindi huo, KCCA imetimiza pointi 60 kutoka mechi 30, moja zaidi ya  SC Victoria University inayoshika nafasi ya pili.
    Hilo ni taji la 10 kwa KCC la Ligi Kuu ya Uganda na sasa mwakani watacheza tena michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, wakati SC Victoria University itaiwakilisha Uganda kwenye Kombe la shirikisho.
    Kocha wa KCCA, George Nsimbe amesema atahakikisha anatimiza malengo ya kutwaa mataji mawili kwa kutwaa pia na Kombe la Ligi, michuano ambayo wametinga fainali na watakutana na SC Victoria University.
    Wakati KCC wametetea ubingwa wao wa Uganda, nchini Tanzania waliokuwa mabingwa watetezi, Yanga SC wamevuliwa taji na Azam FC.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KCC WAFANYA KILE AMBACHO YANGA SC WAMESHINDWA TANZANIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top