// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); TANZANIA YAWEKWA NA NIGERIA, TUNISIA NA UGANDA KUNDI C AFCON 2025 - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE TANZANIA YAWEKWA NA NIGERIA, TUNISIA NA UGANDA KUNDI C AFCON 2025 - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Tuesday, January 28, 2025

    TANZANIA YAWEKWA NA NIGERIA, TUNISIA NA UGANDA KUNDI C AFCON 2025


    TANZANIA imepangwa Kundi C katika Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 zitakazofanyika kuanzia Desemba 21 mwaka huu hadi Januari 18 mwakani, 2026 pamoja na jirani zao, Uganda, Tunisia na Nigeria.
    Katika Droo ya upangaji makundi ya AFCON 2025 iliyofanyika usiku wa Jumatatu ukumbi wa Mohammed V National Theatre Jijini Raba nchini Morocco, wenyeji wa Fainali hizo wapo Kundi A pamoja na Mali, Zambia na Comoro, wakati mabingwa watetezi,  Ivory Coast wapo Kindi F pamoja na Cameroon, Gabon na Msumbiji.
    Kundi B linazikutanisha Misri, Afrika Kusini, Angola na Zimbabwe, wakati D kuja Senegal, DRC, Benin na Botswana na Kundi E wapo Algeria, Burkina Faso, Equatorial Guinea na Sudan.


    MAKUNDI YOTE AFCON 2025 MOROCCO
    KUNDI A: Morocco, Mali, Zambia, Comoro
    KUNDI B: Misri, Afrika Kusini , Angola, Zimbabwe
    KUNDI C: Nigeria, Tunisia, Uganda, Tanzania
    KUNDI D: Senegal, DRC, Benin, Botswana
    KUNDI E: Algeria, Burkina Faso, Equatorial Guinea, Sudan
    KUNDI F: Ivory Coast, Cameroon, Gabon, Msumbiji 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TANZANIA YAWEKWA NA NIGERIA, TUNISIA NA UGANDA KUNDI C AFCON 2025 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top