// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); PLUIJM: YANGA SC NILIKUWA NAPITA TU - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE PLUIJM: YANGA SC NILIKUWA NAPITA TU - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Thursday, May 08, 2014

    PLUIJM: YANGA SC NILIKUWA NAPITA TU

    Na Renatus Mahima, Dar es Salaam
    HANS Van Der Pluijm, kocha mkuu wa Yanga amesema kwamba alikuwa anapita njia tu katika klabu hiyo, kwani muda mrefu alikuwa ana dili la kazi Uarabuni.
    Pluijm amewaaga rasmi wachezaji wake, viongozi, wapenzi  na wanachama wa klabu hiyo baada ya kumaliza mkataba wake wa miezi sita na sasa anakwenda kujiunga na timu Al Shoalah FC iliyoshiriki Ligi Kuu nchini Saudi Arabia.
    Kocha huyo raia wa Uholanzi ambaye ameiongoza Yanga kwa kipindi cha miezi mitano amesema anashukuru kwa sapoti aliyokuwa akiipata kutoka kwa wachezaji, viongozi, wapenzi na wanachama wa timu hii kwa kipindi chote alipokuwa nchini Tanzania tangu Januari mwaka huu.
    Nilikuwa napita tu; Kocha Hans van der Pluijm amesema alikuwa ana dili la kwenda Uarabuni kabla ya kutua Jangwani
    "Najua wengi itawashangaza kuona ninaondoka lakini ukweli ni kwamba nilikuwa na hiyo dili hata kabla ya kuja Yanga, nilikuwa na makubaliano na timu ya Al Shoalah FC, makubaliano ambayo yanaanza mwezi ujao hivyo nilikubaliana na viongozi wa Yanga kuja kufanya kazi kwa kipindi cha miezi sita tu, ninashukuru tumefanya kazi salama na baada ya mkataba huo kuisha nipo tayari kurudi kuja kufanya kazi Tanzania," amesema Pluijm katika mkutano na waandishi wa habari kwenye ofisi za makao makuu ya Yanga jijini Dar es Salaam leo mchana.
    Aidha, Pluijm aliyechukua jukumu la kuinoa Yanga akichukua mikoba ya Mholanzi mwenzake Ernie Brandts aliyetimuliwa baada ya kufungwa 3-1 katika mechi ya 'ndondo' ya 'Nani Mtani Jembe dhidi ya Simba' Desemba 21 mwaka jana, amesema anaipenda Yanga na amejaza fomu kuomba uanachama.
    Kocha huyo anaondoka leo kwenda Ghana kisha kwenda nchini Saudi Arabia tayari kwa kujiandaa na maandalizi ya msimu ujao katika timu hiyo ambayo ataitumikia kwa kipindi cha mwaka mmoja.
    Kuhusu usajili, kocha huyo amesema ameshakabidhi ripoti yake ya kiufundi tangu juzi ambayo viongozi wanaifanyia kazi kisha kabla ya kuwekwa wazi.
    Kwa upande wake, Beno Njovu, katibu mkuu wa Yanga aliyekuwa amefuatana na kocha huyo katika mkutano huo, amesema wameipokea ripoti ya Pluijm na itajadiliwa na Kamti ya Utendaji ya klabu hiyo kabla ya kuanza kufanyiwa kazi huku akieleza kuwa wataifanyia kazi ripoti hiyo ili kumrahisishia kocha mpya ajaye.
     “Tunamshukuru kwa msaada wake ndani ya Yanga. Kwa kiasi kikubwa tutaifanyia kazi ripoti ya Pluijm, kwani ameiona Yanga na anajua upungufu wake na hii itamrahisishia kocha ajaye ambaye haifahamu

    Yanga,” amesema Njovu.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: PLUIJM: YANGA SC NILIKUWA NAPITA TU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top